RICK BOSS KUJA NA FILAMU ITAKAYOONYESHA TUPAC ALIVYODANGANYA KIFO.

Miezi kadhaa imepita tangu kuwepo na uvumi kuwa rappa mkongwe aliyejizolea umaarufu mkubwa Duniani Tupac Amaru Shakur #tupac yupo hai na anaishi nchini Mexico kwa siri.

Leo hii zimeibuka taarifa mpya kuhusu stori hizi ambapo mtengenezaji wa filamu kutoka huko Las Vergas #rickboss amesema kuwa ana mpango wa kutengeneza filamu ambayo itaonyesha jinsi rappa huyo alivyodanganya kifo na kukimbilia Mexico.

Boss amebainisha kuwa japo kuwa sio kweli lakini amedhamiria kufanya hivyo ili kuweka usawa kwa wale wanaoamini kuwa rappa huyo yupo hai na anaishi huko Mexico.

Hata hivyo amesema kuwa bado anasubiri kibali kwa mamlaka zinazohusika ili aweze kuingia kazini na kutengeneza filamu hiyo ambayo imepewa jina Tupac The Great Escape From UMC.

Radio5FmTheOnlyChoice

SisiSoteNiNdugu

Exit mobile version