Maambukizi ya virusi vya corona yapungua China.

In Kimataifa

Kasi ya maambukizi ya virusi vya corona imepungua nchini China, lakini idadi ya maambukizi ya ugonjwa huo unaofahamika kama COVID-19 yamepanda kimataifa na kufikia watu 90,000. Huku kukiwa na zaidi ya visa 2,100 vilivyothibitishwa katika Umoja wa Ulaya, jumuiya hiyo imeongeza kiwango cha kitisho cha virusi hivyo kutoka “cha chini hadi cha wastani” na kukifanya kuwa “cha wastani hadi cha juu.” Italia, ambayo ndiyo nchi iliyoathirika pakubwa barani Ulaya sasa ina zaidi ya visa 2,000, huku watu 52 wakithibitishwa kufa. Idadi ya vifo nchini Marekani imepanda hadi watu sita. Barani Afrika, visa vya kwanza vya virusi hivyo vimeripotiwa Morocco, Tunisia na Senegal. Mawaziri wa fedha kutoka nchi za kundi la G7 wanapanga kuandaa kongamano leo kujadili hatua za kukabiliana na kuongezeka kwa athari ya kiuchumi kutokana na mripuko huo. Shirika la Biashara Duniani – WTO limeonya kuwa janga hilo lina athari kubwa kwa biashara.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WATANZANIA WATAKIWA KUIUNGA MKONO JKT QUEENS

MKUU wa JKT Meja Jenerali RAJABU MABELE, amewataka watanzania kuiunga mkono timu ya JKT Queens inayokwenda kuliwakilisha Taifa na

Read More...

SERIKALI YATOA BIL 424.6 UTEKELEZAJI MIRADI YA TANRODS RUKWA-ENG MWANGA

KATIKA kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu