Siku moja baada ya korea kusema ilikua tayari kuzamisha meli yakubeba ndege za vita,Rais wa China ametaka kuwepo uvumilivu wakati mawasiliano ya simu na rais wa Marekani yakifanyika.

In Kimataifa

Rais wa China Xi Jinping ametaka kuwepo uvumilivu kutoka pande zote wakati wa mawasiliano ya simu na rais wa Marekani Donald Trump siku moja baada ya Korea kusema kuwa ilikuwa tayari kuzamisha meli ya kubeba ndege za vita ya Marekani.

Mawasiliano hayo ya simu ndiyo ya pili kati ya viongozi hao wawili tangu wakutane huko Florida mapema mwezi huu.

Ni ishara ya hofu ya China kuwa msukosuko kati ya Marekani na Korea Kaskazini utasababisha mzozo.

Siku ya Jumapili vyombo vya habari nchini Korea Kaskazini vilisema kuwa jeshi la Korea Kaskazini lilikuwa tayari kuzamisha meli ya Marekani ya USS Carl Vinson, ambayo Marekani inasema itawasili katika rasi ya Korea siku chache zinazokuja.

Meli hiyo ilitumwa na Rais Trump huku onyo ikitolewa kuwa Marekani imepotza uvumilivu kwa mipango ya nuklia ya Korea Kaskazini.

ASANTE KWA KUSIKILIZA MIMI NI ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

One commentOn Siku moja baada ya korea kusema ilikua tayari kuzamisha meli yakubeba ndege za vita,Rais wa China ametaka kuwepo uvumilivu wakati mawasiliano ya simu na rais wa Marekani yakifanyika.

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu