Afariki Dunia baada ya kufukiwa na kifusi 

In Kitaifa

Mtu mmoja amefariki Dunia na wengine Wanane wameokolewa, baada ya kufukiwa na kifusi katika machimbo ya dhahabu ya Shilalo yaliyopo kwenye kata ya Inonelwa wilayani Misungwi mkoani Mwanza.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mwanza, – Jumanne Muliro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa vikosi vya uokoaji vinamtafuta mtu mwingine ambaye anadhaniwa bado amenasa katika kifusi hicho.

Kamanda Muliro amesema kuwa, tukio hilo limetokea saa Saba usiku wa kuamkia hii leo, ambapo watu hao Kumi waliingia katika machimbo hayo kwa ajili ya kufanya kazi zao za uchimbaji kama kawaida.

Amesema kuwa, mara baada ya kuingia kwenye machimbo hayo, kifusi kiliporomoka na kuwafukia ambapo jitihada za uokoaji zilianza mara baada ya tukio hilo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu