Rais wa Tanzania John Joseph Pombe Magufuli,leo amefungua
karakana kuu ya Jeshi la Wananchi Tanzania JWTZ Lugalo
jijini Dar es Salaam, iliyojengwa kwa msaada wa serikali ya
Ujerumani.
Katika tukio hilo serikali ya Ujerumani imewakilioshwa na
balozi wake hapa nchini Bi Reginiacy ambaye alipata nafasi ya
kuzungumza na kutoa ujumbe wake kidogo, kwa kutumia lugha
ya kiswahili.
Baada ya balozi wa Ujerumani kuzungumza alifuatiwa na mkuu
wa majeshi ya ulinzi hapa nchini Gen Venance Mabeyo, ambaye
amezungumzia ujenzi wa karakana hiyo pamoja na gharama
zilizotumika mpaka kukamilika kwake.
Hatimae mgeni rasmi Rais Dkt John Pombe Magufuli, akapata
wasaa wa kuzungumza katika tukio hilo, ambapo pamoja na
mambo mengine ameishukuru sana serikali ya Ujerumani kwa
msaada huo.
Lakini pia rais Magufuli akatumia fursa hiyo kuzungumzia
ugonjwa wa koroma, na kuwataka watanzania kutopuuzia
tahadhari zinazotolewa juu ya ugonjwa huo, na kusitisha safari
za safari za ndege za ATCL kwenda India



