KIGWANGALA ASHUHUDIA UVISHWAJI WA VYEO KWA MAAFISA WAKUU NGORONGORO

In Kitaifa

Waziri wa maliasili na utalii Dr Hamis Kigwangala amewaagiza maafisa wakuu wa mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro na mamlaka nyingine kufanya kazi zao kwa uwadilifu ikiwa ni pamoja na kuzingatia sheria na ili kuweza kukuza na kuendeleza sekta ya utalii hapa nchini.


Ameyasema hayo wakati wa sherehe za uvishwaji vyeo vya jeshi USU kwa manaibu makamishna na makamishna wa hifadhi ya Ngorongoro iliyofanyika katika viwanja wa shule ya msingi Makao Mapya vilivyopo ndani ya hifadhi ya Ngorongoro
Amesema kuwa, amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa sheria ya jeshi USU ambayo taasisi nne ambazo ni TANAPA AMSA TFS na TAWA katika utekelezaji a majukumu yao kutoka mfumo wa kiraia uliokuwa umezoeleka hapo awali nma sasa kufuata mfumo wa Jeshi USU.


“Mfumo wa kuingia jeshi USU umelenga kutekeleza sheria ya wanyamapori no5 ya mwaka 2009 unaoelekeza kubadili mfumo wa uendeshaji kutoka wa kiraia na kuwa wa kijeshi ambao ulizinduliwa rasmi nov 17 mwaka 21019 na Mh. Makamu wa raisi Mama Samia Suluh Hassan ambapo hatua hii ni kutokana na changamato zilizokuwa zikijitokea kwa miaka ya hivi karibuni kama vile ujangili kwa wanyama, na uvamizi wa mifungo kwenye maeneo ya hifadhi”Alisema Kigwangala

Amesema serikali ya awamu ya tanu imedhamiria kuona kuwa sekta ya uhifadhi na ulinzi wa wanyamapori inaboreshqwa kiutendaji ili kukidhi matakwa ya kisheria na kuendana na mbinu za kisayansi na technologia na kuhakikisha maeneo yote yaliyotekwa kwa ajili ya uhifadhi wa wanyamapori na uhifadhi yanalidwa kwa nguvu zote kwa kutoa matokeo chanya na endelevu kwa kuimarisha nidhamu, na ukakamavu uwajibikaji na uwadilifu illi kuongeza ubora katika utendajikazi  kwa watumishi katika ulinzi wa rasilimali za taifa

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la wafugaji mamlaka ya hifadhi Ngorongoro Pr, Abuid Kashamira amefanya zoezi la kuwatunuku vyeo viongozi hao ambapo amesema utekelezaji huo ni wa sheria no 5 ya mwaka 2009 ambapo ni kutoka mfumo wa kiraia kwenda jeshi USU ambayo italeta mabadiliko makubwa na yenye faida katika sekta ya utalii

Amesema kuwa,Vyeo hivyo ni muhimu kwa sababu ya maafisa na maaskari kutambuana, kujenga mtiririko sahihi wa Amri, kujenga nidham ya kijeshi, ukakamavu, ufanisi katika shughuli, na kuongeza na kujenga uzalendo katika kutekeleza majukumu na sheria za maliasili na utalii hapa nchini

Nae inspekta Jeneral Wa Polis  Tanzania IGP Simon Siro amewapongeza makamishna hao kwa kupandishwa vyeo huku akiwataka kutumia vyeo hivyo vizuri na kufanya jeshi kuendelea kuheshimika na kuwa na nidhamu kwa kuzingatia kanuni na sheria

Hata hivyo sherehe hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali na waliopandishwa vyeo ni manaibu kamishna 2 ambao ni uhifadhi maendeleo ya jamii, huduma za shirika, na makamishna wahifadhi wasaidizi waandamizi wa idara mbalimbali za mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu