Marekani yaiwekea vikwazo DR Congo.

In Kimataifa

Serikali ya Marekani imewawekea vikwazo maafisa watatu wa tume ya uchaguzi nchini DR Congo pamoja na wale wa serikali ya aliyekuwa rais wa taifa hilo Joseph kabila kwa tuhuma za ufisadi.

Taarifa iliochapishwa katika mtandao wa wizara ya fedha nchini Marekani, inasema kuwa watatu hao walidaiwa kula rushwa ili kuzuia na kuchelewesha maandalizi ya uchaguzi wa haki na ulioshirikisha pande zote.

Watatu hao ni rais wa tume ya uchaguzi nchini DRC Corneille Yobeluo Nangaa (Nangaa), naibu wake Norbert Basengezi Katintima (Katintima), na mwanawe Katintima, Marcellin Basengezi Mukolo (Basengezi), ambaye ni mshauri mkuu katika tume hiyo ya uchaguzi CENI.

Kulingana na taarifa hiyo iliotiwa saini na katibu wa maswala ya ugaidi na intelijensia ya kifedha nchini Marekani Sigal Mandelker, watuhumiwa hao walifanya vitendo ambavyo vilikandamiza mikakati ya kidemokrasia au taasisi zake nchini DRC.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu