SHEMEJI NI KIKWAZO KWA NYUMBA YANGU.

In Mahusiano

Wenzangu wote natumaini ni wazima leo nami naleta mada kwenye nzito nikitaka kusaidiwa mimi ni mwanaume na nimeoa, bahati mbaya baada ya kuoa wazazi wa mke wangu wote wakafariki akimuacha mke wangu na ndugu zake wa kike wawili ambao hawana kazi wa shule tegemeo lao ilikuwa mama yao na mke wangu dada yao.

Baada ya mama yao kufariki mke wangu akaniomba kama ndugu zake wangeweza kukaa nasi maana walikuwa hawana msaada nikakubali lakini baada ya muda hawa ndugu wa mke wangu naona wananifanyia mambo nisiyoelewa vituko kutwa haviishi ndani.

Ndugu yake mmoja amepata bwana basi yeye kutwa kwa huyo mwanaume hata na kurudi saa sita za usiku hata mimi mwenye nyumba nimeshalala na imetokea mara kwa mara nikimwambia mke wangu amkanye mdogo wake ananiambia kwanini ninawivu na mdogo wake ama namtaka mdogo wake? yani anakuwa mkali kabisa na wala hamwambii mdogo wake, huyu ndugu yake mwengine yeye ni mchafu sana, yani mpaka ananuka anaweza kukaa hata siku nne hajaoga tena akiwa kwenye hedhi ndio balaa ndani hapakaliki juzi kaniacha hoi baada ya kujisaidia haja kubwa kwenye ndoo ya jikoni na kuyaacha ndani.

Vituko vyao nimechoka sasa, nikimwambia mke wangu anasema nataka kuwafukuza wakati najuwa hawana pa kwenda, na inakuwa ugomvi kubwa sana na mke wangu mpaka nashindwa kuelewa ndugu zangu nifanye nini mwenzenu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu