TUME YA MADINI YAZIDI KUIPAISHA SEKTA YA MADINI

In Uchumi

Mnada wa kwanza wa almasi tangu kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika wafanyika..
Wafanyabiashara wa madini wapongeza Wizara ya Madini, Tume ya Madini

Tume ya Madini kupitia Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Shinyanga leo tarehe 18 Februari 2019 imeweka historia ya nchi baada ya kufanya mnada wa asilimia tano ya madini ya Almasi kutoka Mgodi wa Williamson Diamond Limited uliopo mkoani Shinyanga.

Akizungumza kupitia mahojiano maalum, Meneja wa Biashara ya Madini wa Tume ya Madini, George Kaseza amesema kuwa uuzaji wa asilimia tano ya almasi kutoka mgodi wa WDL ni matokeo ya maelekezo yaliyotolewa na Waziri wa Madini, Doto Biteko kupitia mkutano wake alioufanya mwaka jana na wadau wa madini mkoani Shinyanga.

Ameeleza kuwa, kupitia mkutano husika ilikubalika mgodi wa WDL kuuza asilimia tano ya almasi yake kwa wafanyabiashara wadogo wa madini ili waweze kwenda kuuza kwenye Soko la Kimataifa la Dhahabu na Almasi la Shinyanga na kujipatia kipato huku wakilipa kodi mbalimbali Serikalini.

Amesema mgodi wa WDL ulianza kwa kujenga kituo ndani ya eneo lake ambapo kwa kuanzia mnada umeanza kufanyikia hapo.

Kaseza amewataka wafanyabiashara wadogo wa madini ya almasi na dhahabu nchini kuyatumia masoko yaliyoanzishwa hivi karibuni.

Wakizungumza katika nyakati tofauti wafanyabiashara wadogo wa madini ya almasi wamepongeza Serikali kupitia Wizara ya Madini na Tume ya Madini na kuongeza kuwa mbali na kujipatia kipato wataanza kulipa kodi mbalimbali Serikalini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu