WACHEZAJI WA MINZIRO WAPEWA SIKU 10 KULA BATA NA FAMILIA

In Michezo

UONGOZI wa Singida United umeamua kuwapa siku 10 za mapumziko wachezaji wake ili kurejea kwenye familia zao pamoja na kupata muda wa kupumzika kwa muda.

Singida United iliyo chini ya kocha Felix Minziro ilishindwa kubeba pointi tatu kwenye mchezo wake wa mwisho dhidi ya KMC uliochezwa uwanja wa Namfua kwa kugawana pointi mojamoja.

Ofisa Habari wa Singida United, Cales Catemana amesema kuwa ligi imekuwa na ushindani hivyo wameamua kuwapa mapumziko wachezaji wapate akili mpya.

“Tunatambua kwa sasa bado mwenendo wetu haujawa mzuri ila bado tunapambana kurejea kwenye ubora, kwa sasa tumeamua kuwapa mapumziko ya siku 10 wachezaji ili wakirejea wawe na ari mpya.

“Mchezo wetu unaofuata ni dhidi ya Stand United ya Shinyanga hivyo baada ya kurejea kambini tutaanza kujipanga kwa ajili ya mchezo huo,” amesema

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu