Mwanasiasa Elizabeth Warren ametangaza kujiondoa kutoka kwenye mchuano wa kuwania kuteueliwa na chama cha Democratic kuwa mgombea wa kiti cha urais wa Marekani uliopangwa baadae mwaka huu.Warren mwenye umri wa miaka 70 na aliyewahi kuongoza kura za maoni kwenye kinyangányiro hicho, amefikia uamuzi huo baada ya kupata matokeo mabaya ya kura za mchujo kwenye majimbo kadhaa mapema wiki hii.Seneta huyo mpenda mageuzi wa Jimbo Massachusetts amesema anasitisha kampeni yake ya kuwania tiketi ya chama Democratic na kujizuia kutangaza mwanasiasa anayemuunga mkono kwenye mchuano huo.Wakati wa kura za mchujo kwenye majimbo 14 iliyofanyika siku ya Jumanne, Warren alishika nafasi ya tatu nyumba ya Seneta Bernie Sanders na makamu wa rais wa zamani Joe Biden