Mfumo wa leseni za udereva utakuwa na makundi mbalimbali ya madaraja ya leseni za udereva kama ifuatavyo:
Pikipiki
A – Leseni ya kuendesha pikipiki zenye/zisizo na kigari na ambazo injini zake zina ukubwa zaidi ya cc 125 au uzito wa kilo 230.
A1 – Leseni za kuendesha pikipiki zisizo na kigari na ambazo ukubwa wake wa injini ni mdogo kuliko cc 125 au chini ya kilo 230.
A2 – Leseni ya kuendesha pikipiki za magurudumu matatu na manne.
A3 – Leseni za kuendesha pikipiki baiskeli ambazo ukubwa wake wa injini hauzidi cc 50
Vyombo Binafsi vya Moto
B – Leseni ya kuendesha aina zote za vyombo vya moto isipokuwa pikipiki, magari ya biashara, magari makubwa na magari ya kutoa huduma kwa umma.
Magari ya kutoa huduma kwa Umma
C – Leseni ya kuendesha magari ya kutoa huduma kwa umma yenye uwezo wa kubeba abiria 30 na zaidi pamoja na dereva. Magari katika kundi hili yanaweza kufungwa tela lenye ujazo wa juu unaokubalika usiozidi kilo 750. Waombaji wanatakiwa wawe wamewahi kuwa na leseni ya daraja CI au E kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu.
C1 – Leseni ya kuendesha magari ya kutoa huduma kwa umma yenye uwezo wa kubeba abiria 15 lakini wasiozidi 30, abiria pamoja na dereva. Magari katika kundi hili yanaweza kufungwa tela lenye ujazo wa juu unaokubalika usiozidi kilo 750. Waombaji wanatakiwa wawe wamewahi kuwa na leseni ya daraja D kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu.
C- Leseni za kuendesha magari ya kutoa huduma kwa umma yenye uwezo wa kubeba abiria wanne lakini wasiozidi kumi na tano. Magari katika kundi hili yanaweza kufungwa tela lenye ujazo unaokubalika usiozidi kilo 750. Waombaji wanatakiwa wawe wamewahi kuwa na leseni ya daraja D kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu.
C3 – Leseni za kuendesha magari ya kutoa huduma kwa umma yenye uwezo wa kubeba abiria wanne au pungufu akiwemo dereva. Magari katika kundi hili yanaweza kufungwa tela lenye ujazo unaokubalika usiozidi kilo 750. Waombaji wanatakiwa wawe wamewahi kuwa na leseni ya daraja D kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu.
Magari Madogo ya Mizigo ya Biashara
D – Leseni ya kuendesha aina zote za vyombo vya moto isipokuwa pikipiki, magari makubwa na magari ya kutoa huduma kwa umma.
Magari makubwa ya Mizigo ya biashara
E – Leseni ya kuendesha aina zote za vyombo vya moto isipokuwa pikipiki na magari ya umma. Waombaji wanatakiwa wawe wamewahi kuwa na leseni ya daraja D kwa muda usiopungua miaka mitatu.
Magari yenye Trela
F – Leseni ya kuendesha magari yanayokokota trela.
Magari ya Shambani na Migodini
G – Leseni ya kuendesha magari ya shambani na migodini.
Wanaojifunza
H – Leseni ya muda ya kujifunza
