Jean-Pierre Bemba aachiwa huru kwa muda

In Kimataifa

Korti ya Kimataifa ya Uhalifu yenye makao yake mjini The Hague, ICC imemwachia kwa muda aliyekuwa Makamu Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Jean-Pierre Bemba, baada ya kumuondolea hatia wiki iliyopita. Kuachiwa huko kwa muda kunafungamana na tuhuma za kuwahonga mashahidi wakati kesi yake ilipokuwa ikisikilizwa mwaka uliopita, ambayo kesi yake ya rufaa itasikilizwa tarehe 4 mwezi ujao wa Julai. Majaji wa mahakama ya ICC walimruhusu kuondoka katika jela ya mahakama hiyo mjini The Hague, ikiwa ataheshimu masharti magumu aliyowekewa. Mojawapo ya masharti hayo ni kuripoti mara moja kwenye vyombo vinavyohusika akitakiwa kufanya hivyo, kutobadilisha anuani yake bila kuiarifu mahakama, na kujizuia kutoa tangazo lolote hadharani. Wakili wa Bemba Peter Haynes amesema mteja wake ananuia kurejea mjini Brussels kujiunga na familia yake iliyoko huko.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu