Rais wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi ametangaza kifo cha Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad aliyefariki katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam. Rais Dk Mwinyi ametangaza siku saba za maombolezo na bendera kupepea nusu mlingoti.
“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar” amesema Dk Mwinyi