Ronaldo apoteza matumaini ya Juventus kusonga mbele UEFA.

In Kitaifa

Klabu ya Real Madrid jana usiku imeibuka na ushindi mnono wa goli 3-0 dhidi ya Juventus, mchezo uliopigwa nchini Italia na kupoteza kabisa matumaini ya Vizee wa Torino kusonga mbele kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya.

Magoli ya Real Madrid yalifungwa na Cristiano Ronaldo x2 na moja likifungwa na Marcelo kunako dakika 72 .

Kwa matokeo hayo Juventus ina kibarua kigumu cha kupata matokeo ya goli 4-0 au ushindi wowote wa tofauti ya goli 4 ili waweze kusonga mbele  kwenye michuano hiyo kitu ambacho kitakuwa kigumu sana kwao.

Hata hivyo, Juventus itakuwa na wakati mgumu zaidi kwani kwenye mchezo wa marudiano  itamkosa mshambuliaji wake Dyabala baada ya jana kwenye mchezo huo kupata kadi nyekundu.

Matokeo mengine ya jana ni ushindi wa Bayern Munich wa goli 2-1 dhidi ya Sevilla mchezo ambao ulikuwa na msisimko sana kutokana na ugumu wa timu zote mbili kwenye safu ya ulinzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu