Aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya na wenzake 5 wafikishwa mahakamani kwa makosa matano ikiwemo uhujumu uchumi, kuongoza genge la uhalifu,Rushwa , utakatishaji fedha pamoja na unyang’anyi kwa kutumia silaha.
Mashtaka hayo yamesomwa mkurugenzi msaidizi katika ofisi ya taifa ya mashtaka anayeshughulika na usimamizi wa kesi Tumaini Kweka mbele ya Jaji Martha Mahumbuga hakimu mkazi mfawidhi mahakama ya hakimu mkazi Arusha.
Kweka amesema kuwa upelelezi wa makosa yanayowahusisha kesi lengai ole sabaya na wenzake amesema ni tamati ya kuwafikisha mahakamani kutokana na kujiridhisha kwa mkurugenzi na kama Kuna makosa yatajidhihirisha yatapelekwa mahakamani.
Pia kweka amefafanua kuwa wamechelewesha kuwafikisha mahakamani kwasababu ya uchunguzi wa kina na Leo tumewaleta mahakamani kulingana na mashtaka waliyosomewa .
Hata hivyo mashtaka ya pili yamesomwa na Tarsila gervas mbele ya hakimu mkazi mfawidhi mahakama ya arusha Salome mshasha amesema mtuhumiwa lengai ole sabaya, silvester nyagu pamoja Daniel Gabriel mbura wamesomewa kesi ya jinai ya uny’ang’anyi na utumiaji silaha .
Hata hivyo kesi hiyo imeahirishwa ikiwepo ya uhujumu uchumi pamoja na kesi ya uny’ang’anyi ambapo imetajwa kusikilizwa tarehe 18/6 2021 .