Ombi la Barcelona la kumnunua kwa mkopo wa dau la £137m pamoja na kumpatia kandarasi ya kudumu mshambuliaji wa Brazil Neymar, 27, limekataliwa na PSG huku mabingwa hao wa ligue 1 wakiitisha dau la £229m. (Marca)
Manchester United imemfanya winga wa Borussia Dortmund na England Jadon Sancho, 19, lengo lao kubwa katika uhamisho wa mwezi Januari na wanajiandaa kutoa dau la £100m. (Sun)
Liverpool, Manchester City, Manchester United, Arsenal na Chelsea ni miongoni mwa klabu kuu barani Ulaya zinazomlenga mshambuliaji wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Kai Havertz, 20, ambaye ana thamani ya £91m. (Sport1 – in German)#
Beki wa Liverpool na raia wa Croatia asiyehitajika sana Dejan Lovren, 30, anaivutia klabu ya Ujerumani ya Bayer Leverkusen baada ya kufeli kupata uhamisho kuelekea Roma. (Bild – in German)
Tottenham imeanza mazungumzo ya kumuuza kiungo wa kati wa Kenya Victor Wanyama, 28, kuelekea klabu ya Bruges kwa dau la £11m.
Mshambuliaji wa Ubelgiji Michy Batshuayi, 25, anataka kusalia na kupigania nafasi yake Chelsea lakini ataitazama hali mwezi Januari. (Standard)
Manchester City inachunguza hali ya kiungo wa kati wa Argentina na klabu ya Velez Sarsfield Argentine Thiago Almada, 18, ambaye bado hajaandikisha upya kandarasi yake na klabu hiyo.. (A Bola, via Manchester Evening News)