Washtakiwa hao wamefikishwa mahakamani hapo mbele ya hakimu mkazi, Godfrey Mwambapa na kusomewa shtaka la kufanya mkusanyiko usiyo halali na Wakili wa serikali, Faraji Nguka
Baada ya kusomewa kosa hilo washtakiwa walikana ambapo Wakili Nguka ameeleza kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Hata hivyo, Hakimu Mwambapa alitoa masharti ya dhamana kwa washtakiwa ambapo wametakiwa kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini Bondi ya Sh.Milioni 1.5
Washitakiwa hao wamerudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 3, 2018 itakapotajwa.