Yanga yapiga hatua kombe la Shirikisho Afrika,

In Michezo

Yanga SC imefanikiwa kutinga hatua ya kombe la Shirikisho Barani Afrika kwa mara ya pili ndani ya miaka mitatu baada ya kuitoa nje ya mashindano hayo timu ya Welayta Dicha ya Ethiopia hapo juzi kwa jumla ya mabao 2 -1.

Yanga SC ikiwa haina uzoefu wa kutosha kwenye hatua hiyo itakutana na timu nane ambazo nazo zinashiriki kwa mara ya kwanza zikiwemo mbili kutoka Afrika Mashariki.

Viongozi wa CAF wanatarajia kukutana hapo kesho makao makuu ya Shirikisho hilo Cairo, Misri kwaajili ya ratiba ya michuano hiyo.

Timu kutoka ukanda huu wa Afrika Mashariki zilipata nafasi ya kutinga hatua hiyo ni, Yanga SC, Gor Mahia ya Kenya na Rayon Sports ya Rwanda.

Miongoni mwa timu nyinge zilizopata nafasi ya kushiriki kwa mara ya kwanza ni El Masry ya Misri, Wiliamsville kutoka Ivory Cost, Aduana ya nchini Ghana na RS Berkane.

Jumla ya timu zote zilizofanikiwa kuingia hatua ya makundi ni AS Vita (DR Congo), USM Alger (Algeria), El Masry (Egypt), Raja Club Athletic (Morocco), CARA (Congo), El Hilal (Sudan), Gor Mahia (Kenya), UD Songo (Mozambique), Enyimba (Nigeria), Aduana (Ghana), Young Africans (Tanzania), RS Berkane (Morocco), Williamsville (cote d’Ivoire), Djoliba (Mali), Rayon Sports (Rwanda).

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu