Marekani Yaishambulia Syria kwa Makombora

In Kimataifa

Marekani imefanya shambulizi la makombora takriban 50 ,yalipigwa katika kambi ya jeshi la anga mjini Homs nchini Syria.

Awali maafisa wa Marekani walisema wana mpango wa kuchukua hatua za kijeshi baada ya Syria kushutumiwa kutumia silaha za kemikali katika mji unaodhibitiwa na waasi, ambapo watu kadhaa wamepoteza maisha.

Mashambulizi hayo yametekelezwa kutoka kwenye meli za kijeshi za Marekani katika bahari ya Mediterranea.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema ameamuru kutekelezwa kwa mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Syria huku akitoa wito kwa mataifa yote yaliyostaarabika kukomesha vitendo vya mauaji na umwagaji damu nchini humo

Naye mshirika wa Syria Urusi ametahadharisha madhara yatokanayo na hatua zozote za kijeshi zinazochukuliwa na Marekani dhidi ya Syria .

Mike Pregent ni mchambuzi wa masuala ya mashariki ya kati ameiambia BBC kuwa mashambulizi hayo yametoa ujumbe mzito kwa Assad.

Shambulio hilo linawapa Watu wa Syria matumain, na ninachomaanisha ni kuwa haya hakika haya ni Mashambulizi dhidi ya vikosi vya anga vya Assad, silaha za kemikali, pengine dhidi ya hifadhi za mafuta halikadhalika.hivyo haikuwa dhidi ya raia, haikuwaweka marubani wa kimarekani hatarini. Ulikuwa ujumbe maalum kwa Assad kuwa usitumie jeshi lako la anga kuwaadhibu raia, hivyo nafikiri ni ujumbe wenye nguvu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu