URAIS Wamkataa Wassira

In Kitaifa

Mwanasiasa   mkongwe nchini, Stephen Wasira, amesema Rais Samia aachwe amalizie vipindi viwili vya urais kama ilivyo utamaduni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Aliyasema hayo jana mkoani Mara alipopewa nafasi ya kuzungumza baada ya Rais Samia kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa chujio la maji wilayani Bunda.

“Wale waliosema wanataka urais 2025, mimi nawashauri wasubiri kwa sababu kwa utamaduni wa CCM kama kuna rais aliyepo ofisini huwa hatumpingi, tunampa nafasi amalizie awamu hiyo ambayo ni miaka 10,” alisema Wasira.

Alitoa mfano wake binafsi kwamba aliwania urais, lakini hakuupata na sasa kwa kuwa ameshapitwa na umri, amekaa pembeni na hana nia tena ya kuwania.

Wasira aliwataka wenye dhamira hiyo ya urais wasubiri hadi vipindi viwili vya Rais Samia vipite, na iwapo watakuwa wamepitwa na umri waige mfano wake, ambaye amejiunga na wazee wa Mara maana si wote lazima kuwa rais bali ni fursa ya mtu mmoja.

Akiongelea mradi wa maji alimpongeza Rais kwa kuwapatia fedha za mradi huo ulioasisiwa mwaka 1974 na hatua ya jana ndio inakamilisha ujenzi wa mradi huo.

Pia alimshukuru Rais kwa kuwapatia fedha za miradi mingine ya maendeleo ikiwamo kujengea shule, hospitali na maji katika mkoa huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu