Mabadiliko ya hali ya hewa kuleta hasara ya kifedha

In Kimataifa

Benki ya dunia Jumatatu imesema kwamba uchafuzi wa hewa mashariki ya kati pamoja na kaskazini mwa Afrika unasababisha hasara ya dola bilioni 141 za kimarekani kila mwaka.

Kiasi hicho ni takriban asilimia 2 ya mapato ya ndani, wakati ikihimiza umuhimu wa kutochafua mazingira wakati eneo hilo linapojikwamua kutokana na athari za janga la Corona. Ripoti hiyo imeongeza kusema kwamba uchafuzi wa mazingira utagharimu baadhi ya mataifa kwenye eneo hilo kama vile Misri,Lebanon na Yemen zaidi ya asilimia 3 ya mapato ya ndani kila mwaka.

Uzalishaji wa nchi hushuka pale wakazi wanaposhindwa kufanya kazi kutokana na maradhi yaliyosababishwa na uchafuzi wa hewa, wakati gharama ya matibabu ikiwa mzigo mkubwa kwa watu binafsi au hata serikali,ripoti hiyo imeongeza.

Takwimu zinaonyesha kwamba mtu wa kawaida huenda akapoteza siku 60 za maisha yake wakati akiugua kutokana na uchafuzi wa hewa, wakati wakazi wa mijini wakisemekana kuvuta uchafu mara 10 juu ya viwango vinavyosemekana kuwa salama kutoka shirika la Afya duniani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu