Rais Samia aweka shada Kaburi la Mashujaa Urusi

In Kimataifa

Rais Samia Suluhu Hassan leo ameweka shada la maua katika Kaburi la Mashujaa jijini Moscow Urusi kwa heshima ya wananchi na askari zaidi ya milioni 20 waliopoteza maisha wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia.

Rais Samia yuko katika ziara ya kitaifa ya siku tatu nchini Russia ambalo leo mchana anatarajiwa kukutana na mwenyeji wake, Rais Vladimir Putin, katika Ikulu ya Kremlin jijini Moscow.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa kabla ya mkutano huo, viongozi hao wawili wanatarajiwa kuzungumza kwa kina kuhusu masuala anuai yakiwemo biashara, uchumi, uwekezaji na kilimo.

Kesho Rais Samia ataongoza mkutano wa wafanyabiashara wa Tanzania na Russia na pia kuzungumza katika Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi utakaofanyika katika jiji la St. Petersburg.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu