Ali Reza Akbari ahukumiwa kifo

In Kimataifa

Iran imemuhukumu kifo afisa mkuu wa zamani wa ulinzi baada kumkuta na hatia kwa mashtaka ya kuifanyia ujasusi Uingereza, chombo cha habari chenye uhusiano na serikali kimeripoti Jumatano.

Mahakama imesema Ali Reza Akbari, ambaye alikuwa naibu waziri wa ulinzi hadi mwaka 2001, alikuwa “jasusi mkuu” wa idara ya ujasusi ya Uingereza, shirika la habari la Tasmin limeripoti.

Tasmin imeripoti pia kuwa alifanya ujasusi kwenye mazungumzo ya zamani ya nyuklia kati ya Iran na mataifa ya magharibi.

Akbari alihudumu kama naibu waziri wa ulinzi chini ya uongozi wa Rais Mohammad Khatami, mwanamageuzi ambaye alishinikiza kuboreshwa kwa uhusiano na nchi za magharibi.

Uingereza imeomba hukumu hiyo isitishwe na Akbari aachiliwe mara moja.

Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza James Cleverly amesema katika taarifa “ Hiki ni kitendo kilichochochewa kisiasa na utawala wa kikatili ambao unapuuza kabisa maisha ya binadamu.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu