Benki ya Dunia yatoa mikopo ya kupambana na COVID-19

In Kimataifa

Benki ya Dunia imetangaza kuwa inatoa mara moja mikopo ya dola bilioni 12 kwa nchi zinazooendelea, kusaidia kupambana na virusi vya corona ambavyo vimesambaa kutoka China hadi nchi 80 duniani. Rais wa Benki ya Dunia David Malpass amesema lengo ni kutoa msaada wa haraka wa kukabiliana na athari za kiafya na kiuchumi zinazosababishwa na janga la COVID 19. Nchi maskini hazina vifaa vizuri vya kuzuia kusambaa kwa virusi vya ugonjwa huo. Fedha hizo huenda zikatumika katika utanuzi wa mifumo ya afya miongoni mwa mambo mengine. Benki ya Dunia siku za nyuma ilizindua mifuko ya msaada wakati wa majanga kama vile Ebola au Zika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Rais Samia aweka shada Kaburi la Mashujaa Urusi

Rais Samia Suluhu Hassan leo ameweka shada la maua katika Kaburi la Mashujaa jijini Moscow Urusi kwa heshima ya

Read More...

JKT yawaita wahitimu Form 6 2026 kujiunga na mafunzo ya lazima

Jeshi la Kujenga Taifa limewataka vijana wote waliohitimu kidato cha sita mwaka 2026 kutoka shule zote za Tanzania

Read More...

Arsenal Hatimaye Watwaa Taji la Premier League Baada ya Miaka 22 ya KusubiriNa Semio Sonyo – Radio 5

Klabu ya Arsenal hatimaye imeandika historia mpya kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England (Premier League) baada ya kusubiri

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu