Waziri mkuu wa Ukraine ajiuzulu

In Kimataifa

Waziri Mkuu wa Ukraine Oleksiy Honcharuk amewasilisha barua yake ya kujiuzulu kwa mara ya pili katika miezi miwili. Wabunge kutoka chama tawala wataamua leo kama watakubali kujiuzulu kwake au la wakati wa kikao maalum. Waziri wa fedha na mambo ya nchi za kigeni huenda pia wakaondolewa katika nyadhifa zao kama sehemu ya mabadiliko ya baraza la mawaziri. Naibu Waziri Mkuu Denys Shmygal anapigiwa upatu kuchukua nafasi ya Honcharuk. Shmygal awali alihudumu kama mkuu wa utawala wa kikanda katika jimbo la magharibi la Ivano-Frankvisk kabla ya kuchukua wadhifa wa naibu waziri mkuu mwezi uliopita. Hakukuwa na kauli ya mara moja kutoka kwa Honcharuk au Rais Volodymyr Zelenskiy. Haijafahamika wazi kilichomfanya Honcharuk kuwasilisha barua ya kujiuzulu kwa mara ya pili.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Rais Samia aweka shada Kaburi la Mashujaa Urusi

Rais Samia Suluhu Hassan leo ameweka shada la maua katika Kaburi la Mashujaa jijini Moscow Urusi kwa heshima ya

Read More...

JKT yawaita wahitimu Form 6 2026 kujiunga na mafunzo ya lazima

Jeshi la Kujenga Taifa limewataka vijana wote waliohitimu kidato cha sita mwaka 2026 kutoka shule zote za Tanzania

Read More...

Arsenal Hatimaye Watwaa Taji la Premier League Baada ya Miaka 22 ya KusubiriNa Semio Sonyo – Radio 5

Klabu ya Arsenal hatimaye imeandika historia mpya kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England (Premier League) baada ya kusubiri

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu