Boko Haram yawaachia huru wanafunzi wa kike Nigeria.

In Kimataifa
Serikali ya Nigeria imethibitisha kuwa wengi kati ya wanafunzi wa kike 110 waliokuwa wametekwa na kikundi cha Boko Haram zaidi ya mwezi mmoja uliopita wameachiwa Jumatano asubuhi.
Shirika la habari la AFP limeripoti kuwa wasichana hao waliletwa katika mji wa Dapchi ulioko upande wa Kaskazini mwa Nigeria wa Jimbo la Yobe baada ya wale waliokuwa wanawashikilia kuwarejesha katika msafara ulioandamana na magari 9.
Ripoti za vyombo vya habari zimesema wasichana watano kati ya hao walikufa wakati wakisafirishwa, lakini afisa wa serikali wa jimbo la Yobe amesema hili bado halijaweza kuthibitishwa.
Waziri wa Habari wa Nigeria Lai Mohammed amesema kuachiwa kwa wasichana hao mapema asubuhi “bila masharti” kulitokana na “juhudi za kisiri” zikisaidiwa na “baadhi ya marafiki wa nchi hiyo.”
“Wasichana 91 na mvulana mmoja wameelezewa kuwa wameachiwa. Hayo ndio yaliyojiri,” amewaabia waandishi.
“Wengi kati ya wasichana hao, wengi wa wanafunzi hao walioachiwa huru hawakuletwa wote sehemu moja. Waliachwa njiani na wao wenyewe walirudi majumbani kwa wazazi wao.
Vyanzo vya habari nchini Nigeria vimetoa habari kuwa wakazi wa eneo la Dapchi walikuwa wanafurahia kuachiwa kwa watoto hao.
Wazazi ambao hapo awali walikuwa wanamsiba kwa kutekwa kwa vijana wao hivi sasa wanasheherekea kurudi kwao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu