CONGO YAWARUHUSU UGANDA KUWASHAMBULIA WAASI

In Kimataifa

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kwamba serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imewaruhusu wanajeshi wa Uganda UPDF, kuingia sehemu zaidi ambazo waasi wa kundi la Allied Democratic Forces ADF wanaaminika kujificha, na kuwashambulia waasi hao.

Katika ujumbe wa Twitter, Museveni amesema kwamba jeshi la Uganda limeruhusiwa kutekeleza mashambulizi nje ya Kivu Kaskazini, na kuua mamia ya waasi wa ADF.

“Ijumaa Novemba 4, 2022, kwa ruhusa ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wanajeshi wa Uganda walishambulia kambi kubwa ya ADF,” ameandika Museveni akiongezea kwamba “adui sasa amekimbia na kuondoka nje ya mipaka yetu tunayoruhusiwa kumshambulia. Magaidi wapumbavu hawajui kwamba tunaweza kuwafikia katika muda wa dakika chache sana na wala sio masaa na kuwashambulia kwa moto mkali sana hata nje ya sehemu tunayoruhusiwa kufanya kazi.”

Museveni amebandika video ya shambulizi la jeshi la Uganda, kwenye ujumbe wake wa Twitter.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu