Dkt Samia: Napunguza msafara wangu kupunguza matumizi ya mafuta

In Kitaifa

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametangaza mpango wa kupunguza ukubwa wa msafara wake, ikiwa ni hatua za mwanzo za kukabili matumizi ya mafuta, kutokana na kupanda kwa bei ya nishati hiyo duniani.

Katika utekelezaji wa hilo, Dkt Samia amesema wakuu mbalimbali wa idara wanaoongozana naye katika misafara hiyo wakiwa na magari yao, kwa sasa wote watapanda kwenye basi moja na kuacha magari yao.

Dkt Samia ametoa kauli hiyo Ikulu jijini Dodoma leo, Jumatano Aprili 8, 2026, alipohutubia baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua wiki iliyopita.

“Msafara utakuwa gari yangu, escort yangu ya polisi na gari ya akiba nyuma, waliobakia wote nawaingiza kwenye basi tupunguze matumizi ya mafuta,” amesema.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

TUMUOMBEE RAIS, TULIOMBEE TAIFA-MASHILI

Na Mwandishi Wetu, Tabora.WATANZANIA wamehamasishwa kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili

Read More...

RC MAKALLA AKUTANA NA BABA ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI ARUSHA

. Rc Makalla aomba Kanisa na viongozi wa dini zote kuendelea kuiombea nchi Amani na utulivu . Askofu Isaac Amani

Read More...

Serikali yatangaza hatua kuhakikisha mafuta yanapatikana

Serikali imetangaza kuchukua hatua madhubuti za kuhakikisha upatikanaji endelevu wa mafuta nchini, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuikinga

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu