Katibu wa Kanda ya Kaskazini ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake pamoja na kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuanzia leo tarehe 01 Aprili 2026.
Katika taarifa yake, kiongozi huyo ameeleza kuwa uamuzi huo umetokana na majukumu mapya aliyoyapata, ambayo yanamlazimu kujiondoa katika nafasi ya uongozi na uanachama wa chama hicho.
Aidha, ametoa shukrani za dhati kwa Kamati Kuu ya chama kwa imani kubwa waliomuonyesha katika kipindi chote cha utumishi wake. Pia amemshukuru kiongozi aliyekuwa akifanya naye kazi kwa ushirikiano mzuri, pamoja na viongozi na wanachama wote wa Chadema Kanda ya Kaskazini kwa msaada na ushirikiano waliompatia.
Akihitimisha, amewatakia viongozi na wanachama wote wa chama hicho mafanikio mema katika harakati za kuendeleza demokrasia nchini.



