Katibu wa Kanda ya Kaskazini Ajiuzulu na Kujivua Uanachama Chadema

In Kitaifa

Katibu wa Kanda ya Kaskazini ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake pamoja na kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuanzia leo tarehe 01 Aprili 2026.

Katika taarifa yake, kiongozi huyo ameeleza kuwa uamuzi huo umetokana na majukumu mapya aliyoyapata, ambayo yanamlazimu kujiondoa katika nafasi ya uongozi na uanachama wa chama hicho.

Aidha, ametoa shukrani za dhati kwa Kamati Kuu ya chama kwa imani kubwa waliomuonyesha katika kipindi chote cha utumishi wake. Pia amemshukuru kiongozi aliyekuwa akifanya naye kazi kwa ushirikiano mzuri, pamoja na viongozi na wanachama wote wa Chadema Kanda ya Kaskazini kwa msaada na ushirikiano waliompatia.

Akihitimisha, amewatakia viongozi na wanachama wote wa chama hicho mafanikio mema katika harakati za kuendeleza demokrasia nchini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

TUMUOMBEE RAIS, TULIOMBEE TAIFA-MASHILI

Na Mwandishi Wetu, Tabora.WATANZANIA wamehamasishwa kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili

Read More...

JCB Ailipua Media, “Hip Hop Inabaniwa Redioni, Wasanii Wachache Wapewa Nguvu Zote!”

Msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop nchini, JCB, anayetoka kundi la Watengwa, ameeleza wasiwasi wake kuhusu mwenendo wa

Read More...

Serikali yatangaza hatua kuhakikisha mafuta yanapatikana

Serikali imetangaza kuchukua hatua madhubuti za kuhakikisha upatikanaji endelevu wa mafuta nchini, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuikinga

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu