ECOWAS kukutana Abuja kujadili mapinduzi nchini Niger.

In Kimataifa

Wakuu wa majeshi ya nchi wanachama wa jumuia ya uchumi ya mataifa ya Afrika magharibi (ECOWAS) wanakutana katika mji mkuu wa Nigeria Abuja kuanzia leo Jumatano hadi Ijumaa kujadili mapinduzi ya kijeshi nchini Niger, jumuiya hiyo imesema.

Siku ya Jumapili, ECOWAS iliiwekea vikwazo Niger na kuonya kuwa inaweza kutumia nguvu huku ikiupa utawala wa kijeshi muda wa wiki moja kumrejesha madarakani Rais Mohamed Bazoum.

Afisa wa ECOWAS pia aliiambia AFP jana Jumanne kwamba ujumbe wa jumuiya hiyo unaoongozwa na rais wa zamani wa Nigeria Abdulsalami Abubakar utafanya ziara Niger leo Jumatano.

Mapinduzi hayo yamezitia wasiwasi nchi za magharibi zinazojitahidi kudhibiti uasi wa wanamgambo wa kiislamu uliozuka kaskazini mwa Mali mwaka 2012, na kuingia Niger na Burkina Faso miaka mitatu baadaye na sasa unatishia mataifa dhaifu katika Ghuba ya Guinea.

Raia kadhaa, wanajeshi na polisi wameuawa katika eneo hilo lote, wengi katika mauaji ya kikatili, huku watu milioni 2.2 nchini Burkina Faso pekee wakiwa wamehama makazi yao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu