Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limekamata gari aina ya Toyota
Harrier ikiwa imebeba bunda elfu 1 na 50 za mirungi sawa na
kKilogramu 561.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ramadhani Ng’anzi
amesema kuwa,gari hiyo mali ya Malema Maswi yenye namba
za usajili T161 DGP ilikamatwa Juni 8, 2022 Saa 5: 20 usiku
katika maeneo ya Itumbili wilayani Magu mkoani Mwanza.
Ameeleza kuwa ilikamtwa baada ya kutelekezwa na dereva
ambaye jina lake halijatambulika.



