KATIBA YA CCM YAFANYIWA MABADILIKO 

In Kitaifa, Siasa

Kwa mujibu wa taarifa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi na kufanya mabadiliko madogo katika Katiba ya CCM ambapo sasa Katiba hiyo inatambua ufanywaji wa mikutano ya ngazi mbalimbali kwa njia ya mtandao maarufu kama E- Meeting.

Dkt. Samia wakati akitangaza mapendekezo hayo kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, Mabadiliko hayo ni katika kuhakikisha kuwa Chama hicho kinaenda sawa na mabadiliko mbalimbali ya teknolojia yanayotokea duniani,suala ambalo limewezesha CCM pia kufunga Mitambo ya teknolojia yenye kuwezesha Ngazi za CCM wilaya na Mikoa kuweza kuunganishwa pamoja na Makao Makuu kwa njia ya mtandao.

Amebainisha kuwa Idara ya Oganaizesheni ilipendekeza vikao vitakavyoweza kufanyika kimtandao ni Vikao vya Sekretarieti ya Wilaya, Kamati za siasa za wilaya, Sekretarieti za Mikoa, Kamati za siasa za Mikoa, sekretarieti ya Kamati maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Kamati Maalum ya halmashauri kuu ya CCM Taifa,Halmashauri kuu ya CCM Taifa pamoja na Mkutano Mkuu wa Taifa.

“Vikao husika vitafanyika kwa njia ya mtandao endapo tu kuna ulazima, vikao husika kwa ngazi ya Mkoa vitafanyika kwa idhini ya Katibu Mkuu. Watamjulisha Katibu Mkuu kwanini wafanye kikao kwa mtandao na hii ni kuepusha kutumika vibaya kwa mitandao hii.” Ameongeza Dkt. Samia.

Mabadiliko mengine ya Katiba yaliyofanywa na Mkutano Mkuu wa CCM Leo Alhamisi ni pamoja na Kuongeza idadi ya mabaraza ya wadhamini kutoka nane hadi tisa pamoja na mabadiliko madogo ya kutaka miradi ya maendeleo inayotekelezwa ngazi ya Mikoa kukasimiwa kwa maandishi kwenye ngazi hizo.

ReplyForwardAdd reaction

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu