Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania anaitwa
Padri Dr. Charles Kitima amefafanua tamko la Kanisa Katoliki
kuzuia watu kufunga ndoa nakusema hawajazuia sakramenti
hiyo ila wamezuia wale wanaotaka kufanya sherehe.
Dr. Charles amesema Ibada ya kupokea Sakrament ya ndoa na
kipaimara hizi shughuli zisiandamane na shamrashamra,
ukishafunga ndoa kusiwepo sherehe, kinachofanyika ni
mkusanyiko wa Ibada, kama unataka na sherehe subirisha.
Pia amesema Ndoa zinaendelea kufungwa, mtu amekaribia kufa
huwezi mnyima Ubatizo, nyie Wachumba mmepanga kufunga
ndoa April njooni Kanisani mtafunga mko wawili na
wasimamizi wanne, distance mita moja moja lakini hamna
sherehe.



