Makamu wa Rais aagiza wakandarasi wa ndani kupewa miradi.

In Kitaifa

  Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameagiza miradi yote yenye thamani ya ujenzi isiyozidi bilioni 10 ,wapewe Wakandarasi wa ndani ili kukuza pato la taifa.

Akifungua mkutano wa mashauriano wa Bodi ya usajili wa makandarasi wa mwaka 2017,mjini Dodoma  Amesema kuwa wakandarasi hao wapewe miradi hiyo, ili waweze kuzalisha ajira kwa vijana wengi wa kitanzania waliopo mtaani.

Aidha samia amesema kuwa Serikali itaendelea kuwapa kipaumbele wakandarasi wazawa ,ili wamudu zabuni za ujenzi kwani kwa kufanya hivyo kutaleta faida mbalimbali ikiwemo fedha watakazopata, kwani wataweza kuwekeza ndani ya nchi na kutoa ajira.

Naye Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa kuwa Wizara hiyo inaendelea kusimamia sheria na maadili kwa wakandarasi ili kuhakikisha miradi ya ujenzi inayotekelezwa kote inakuwa na ubora unaotakiwa.

Kwa upande wake, Msajili wa Bodi ya Wakandarasi Nchini, Rhoben Nkori amesema bodi hiyo imefuta usajili wa wakandarasi 3,000 kwa kushindwa kutimiza matakwa ya Usajili wa Wakandarasi ya mwaka 1997 na kwa sasa bodi hiyo inawakandarasi 9,000 kote nchini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu