Makamu wa Rais aagiza wakandarasi wa ndani kupewa miradi.

In Kitaifa

  Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameagiza miradi yote yenye thamani ya ujenzi isiyozidi bilioni 10 ,wapewe Wakandarasi wa ndani ili kukuza pato la taifa.

Akifungua mkutano wa mashauriano wa Bodi ya usajili wa makandarasi wa mwaka 2017,mjini Dodoma  Amesema kuwa wakandarasi hao wapewe miradi hiyo, ili waweze kuzalisha ajira kwa vijana wengi wa kitanzania waliopo mtaani.

Aidha samia amesema kuwa Serikali itaendelea kuwapa kipaumbele wakandarasi wazawa ,ili wamudu zabuni za ujenzi kwani kwa kufanya hivyo kutaleta faida mbalimbali ikiwemo fedha watakazopata, kwani wataweza kuwekeza ndani ya nchi na kutoa ajira.

Naye Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa kuwa Wizara hiyo inaendelea kusimamia sheria na maadili kwa wakandarasi ili kuhakikisha miradi ya ujenzi inayotekelezwa kote inakuwa na ubora unaotakiwa.

Kwa upande wake, Msajili wa Bodi ya Wakandarasi Nchini, Rhoben Nkori amesema bodi hiyo imefuta usajili wa wakandarasi 3,000 kwa kushindwa kutimiza matakwa ya Usajili wa Wakandarasi ya mwaka 1997 na kwa sasa bodi hiyo inawakandarasi 9,000 kote nchini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu