Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya
Rushwa na Uhujumu ikifahamika kama Mahakama ya Mafisadi
Elinaza Luvanda, amejitoa kusikiliza kesi ya Mwenyekiti wa
CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake.
Jaji Luvanda amejitoa baada ya Freeman Mbowe kusimama
mahakamani hapo na kusema kuwa, hana imani na jaji huyo na
kumtaka ajitoe kusikiliza kesi hiyo ili kulinda heshima yake
heshima ya mahakama.