Mashoga wapo salama LUGOLA.

In Kitaifa
Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Kangi Lugola amesema kuwa wapenzi wa jinsia moja hawapo hatarini nchini humo.

Lugola amesema japo ushoga ni kosa la jinai nchini Tanzania, wanaojihusha na vitendo hivyo hawatishiwi maisha na wala hawaikimbii nchi.

Akizungumza na gazeti la serikali la Habari Leo, Lugola amekanusha kuwa wapenzi wa jinsia moja wapo hatarini.

“Ninachosema ni kuwa Tanzania ni salama na hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kuwa sio salama bila ya kuwa na vigezo husika, kama mtu yeyote anahatarishiwa maisha yake, basi anapaswa kwenda Polisi na mimi sijapata taarifa zozote kutokea Polisi zinazoelezea kuwapo kwa mazingira hatarishi ya watu hao,” alisema.
Alisisitiza kuwa kwa upande wa mashoga, hajapata taarifa kutoka kituo chochote cha Polisi nchini, wakilalamikia usalama wao.
Alisema kama kungekuwa na mazingira sio salama kwao, wangeenda kupeleka malalamiko yao kwenye vituo vya Polisi jirani; na kuwa akiwa waziri mwenye dhamana, hajapata taarifa za mazingira hatarishi kwa mashoga nchini.
Hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliwataka wananchi kumtajia majina ya mashoga wa Dar es Salaam, kwa njia ya simu yake ya mkononi.
Kutokana na agizo hilo, watu kadhaa wamekuwa wakiendelea kumtajia majina hayo, hali ambayo imesababisha taharuki kwa baadhi ya watu waliotajwa, huku wengine wakilalamikia utaratibu huo, hasa mashirika ya haki za binadamu yakiwamo ya nje ya nchi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu