Mganga mkuu wa jiji la Dar es salaam Dkt Rashidi Mfaume
ametoa taarifa ya mwenendo wa utoaji wa chanjo ya Uviko19
katika jiji hilo akieleza kuwa,kitakwimu bado wapo chini na
hamasa inahitaji ili kufikia lengo.
Dkt Rashidi Mfaume ameeleza hayo katika kikao kilichohusisha
wadau wa Afya katika jiji la Dar es salaam kilicholenga kupeana
taarifa mbali mbali zikiwemo za namna ya kukabiliana na wimbi
la nne la Uviko 19.
Katika maelezo yake Dkt Mfaume ameelezea kupokelewa kwa
Dozi nyingine za chanjo za Johnson &Johnson,hivyo kuwataka
wananchi waliokuwa wakiulizia chanjo hiyo kufika katika vituo
vya Afya maeneo mbali mbali kupatiwa huduma hiyo.



