Misri yasaini makubaliano na kampuni za China katika kujenga reli nyepesi.

In Kimataifa

Wizara ya usafiri ya Misri imesaini makubaliano na kampuni za China katika kujenga reli nyepesi ya kasi yenye thamani ya dola bilioni 1.24 za kimarekani katika maeneo mapya mjini Cairo.

Reli hiyo mpya yenye urefu wa kilomita 66 na vituo 11, itaunganisha mji mkuu mpya wa utawala unaoendelea kujengwa na maeneo ya Cairo Kuu.

Waziri mkuu wa Misri Bw Sherif Ismail, waziri wa usafiri Bw Hesham Arafat pamoja na balozi wa China nchini Misri Bw Song Aiguo wamehudhuria hafla ya kusaini makubaliano kati ya Shirika la Usafiri la Misri NAT na kampuni ya usafiri wa anga ya China AVIC INTL na kampuni ya reli ya China.

Mkurugenzi wa shirika la usafirishaji la Misiri NAT amesema mradi wa reli hiyo utaanza ndani ya miezi miwili au mitatu, na inatarajiwa kusafirisha abiria laki 3.4 kwa siku.

Kampuni ya China, imesema ujenzi wa reli hiyo utatoa nafasi nyingi za ajira kwa Wamisri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu