Misri yasaini makubaliano na kampuni za China katika kujenga reli nyepesi.

In Kimataifa

Wizara ya usafiri ya Misri imesaini makubaliano na kampuni za China katika kujenga reli nyepesi ya kasi yenye thamani ya dola bilioni 1.24 za kimarekani katika maeneo mapya mjini Cairo.

Reli hiyo mpya yenye urefu wa kilomita 66 na vituo 11, itaunganisha mji mkuu mpya wa utawala unaoendelea kujengwa na maeneo ya Cairo Kuu.

Waziri mkuu wa Misri Bw Sherif Ismail, waziri wa usafiri Bw Hesham Arafat pamoja na balozi wa China nchini Misri Bw Song Aiguo wamehudhuria hafla ya kusaini makubaliano kati ya Shirika la Usafiri la Misri NAT na kampuni ya usafiri wa anga ya China AVIC INTL na kampuni ya reli ya China.

Mkurugenzi wa shirika la usafirishaji la Misiri NAT amesema mradi wa reli hiyo utaanza ndani ya miezi miwili au mitatu, na inatarajiwa kusafirisha abiria laki 3.4 kwa siku.

Kampuni ya China, imesema ujenzi wa reli hiyo utatoa nafasi nyingi za ajira kwa Wamisri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu