Misri yasaini makubaliano na kampuni za China katika kujenga reli nyepesi.

In Kimataifa

Wizara ya usafiri ya Misri imesaini makubaliano na kampuni za China katika kujenga reli nyepesi ya kasi yenye thamani ya dola bilioni 1.24 za kimarekani katika maeneo mapya mjini Cairo.

Reli hiyo mpya yenye urefu wa kilomita 66 na vituo 11, itaunganisha mji mkuu mpya wa utawala unaoendelea kujengwa na maeneo ya Cairo Kuu.

Waziri mkuu wa Misri Bw Sherif Ismail, waziri wa usafiri Bw Hesham Arafat pamoja na balozi wa China nchini Misri Bw Song Aiguo wamehudhuria hafla ya kusaini makubaliano kati ya Shirika la Usafiri la Misri NAT na kampuni ya usafiri wa anga ya China AVIC INTL na kampuni ya reli ya China.

Mkurugenzi wa shirika la usafirishaji la Misiri NAT amesema mradi wa reli hiyo utaanza ndani ya miezi miwili au mitatu, na inatarajiwa kusafirisha abiria laki 3.4 kwa siku.

Kampuni ya China, imesema ujenzi wa reli hiyo utatoa nafasi nyingi za ajira kwa Wamisri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu