Leo tarehe 20 Februari, 2020 mnada wa asilimia tano ya madini ya almasi kutoka katika Mgodi wa Williamson Diamond Limited (WDL) umeendelea kupamba moto baada ya wadau wengi wa madini kuendelea kujitokeza.
Akizungumza kupitia mahojiano maalum, Meneja wa Biashara ya Madini wa Tume ya Madini, George Kaseza amesema kuwa kumekuwepo na mwitikio mkubwa kwenye uwasilishaji wa zabuni mbalimbali katika kituo cha ununuzi wa madini cha Mwadui (Mwadui Buying Centre)
Mnada huo umeanza tangu tarehe 18 Februari, 2020 ambapo wanunuzi wadogo wa madini ya almasi wananunua madini hayo na kwenda kuuza kwa wauzaji wakubwa wa madini waliopo katika Soko la Kimataifa la Dhahabu na Almasi lililopo Shinyanga Mjini.