Mpango wa kudhibiti utoaji wa visa za kazi kwa wageni nchini Marekani kupitiwa upya.

In Kimataifa

Rais wa Marekani aliamua Jumanne hii usiku kutia saini amri ya kupitia upya mpango wa kudhibiti utoaji wa visa za kazi kwa wageni nchini Marekani maarufu kama H-1B. Lakini bunge la Congress litakabiliwa na kibarua kigumu kwa kupitisha sheria hiyo. Wabunge ndio wana uwez0 wa kuidhinisha au la sheria hiyo.

Rais Trump alichagua jimbo la Wisconsin, ambalo linakabiliwa na mdororo wa kiuchumi,akiomba kuwekeza katika jimbo hilo na kuajiri kwanza raia wa Marekani kabla ya mtu yeyote. Alitoa hotuba yake mbele ya bendera ya American katika jimbo la Wisconsin.

Sheria hii inayataka mashirika kufuata taratibu za Serikali katika kuondoa wafanyakazi wa kigeni kwenye mpango wa kuwania zabuni kwenye miradi ya serikali.

Sheria hii ina nia ya kutimiza ahadi yake aliyoitoa wakati wa Kampeni ya ”Marekani kwanza”.

Trump atatoa maelekezo kwa idara ya mambo ya ndani, sheria, usalama wa ndani na kazi na kupendekeza kufanyia mabadiliko mpango huo, ambao unawaruhusu waajiri nchini humo kuwapa wageni nafasi za kazi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu