Mpango wa kudhibiti utoaji wa visa za kazi kwa wageni nchini Marekani kupitiwa upya.

In Kimataifa

Rais wa Marekani aliamua Jumanne hii usiku kutia saini amri ya kupitia upya mpango wa kudhibiti utoaji wa visa za kazi kwa wageni nchini Marekani maarufu kama H-1B. Lakini bunge la Congress litakabiliwa na kibarua kigumu kwa kupitisha sheria hiyo. Wabunge ndio wana uwez0 wa kuidhinisha au la sheria hiyo.

Rais Trump alichagua jimbo la Wisconsin, ambalo linakabiliwa na mdororo wa kiuchumi,akiomba kuwekeza katika jimbo hilo na kuajiri kwanza raia wa Marekani kabla ya mtu yeyote. Alitoa hotuba yake mbele ya bendera ya American katika jimbo la Wisconsin.

Sheria hii inayataka mashirika kufuata taratibu za Serikali katika kuondoa wafanyakazi wa kigeni kwenye mpango wa kuwania zabuni kwenye miradi ya serikali.

Sheria hii ina nia ya kutimiza ahadi yake aliyoitoa wakati wa Kampeni ya ”Marekani kwanza”.

Trump atatoa maelekezo kwa idara ya mambo ya ndani, sheria, usalama wa ndani na kazi na kupendekeza kufanyia mabadiliko mpango huo, ambao unawaruhusu waajiri nchini humo kuwapa wageni nafasi za kazi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu