Rasmi sasa uchaguzi Mkuu wa Uingereza kufanyika.

In Kimataifa

Ni rasmi sasa uchaguzi Mkuu wa Uingereza utafanyika Juni nane mwaka huu. Hii ni baada ya wabunge kuunga mkono hoja ya Waziri Mkuu Theresa May kufanya uchaguzi wa mapema.

Bunge la Uingereza limeunga mkono kwa kura 522 dhidi ya 13. Vyama vya upinzani vimeunga mkono hoja ya Waziri Mkuu.

Bi Theresa May, ametaka idhini kutoka kwa raia wa Uingereza katika kuendeleza mazungumzo ya mchakato wa Uingereza kuondoka Muungano wa Ulaya.

Kiongozi wa upinzani Jeremy Corbyn ameunga mkono uchaguzi wa mapema huku akimlaumu Waziri Mkuu kwa kutotekeleza ahadi zake kwa raia.

Uchaguzi Mkuu wa Uingereza ulipangwa kufanyika mwaka wa 2020. Hata hivyo bunge linaweza kufanyia sheria ya uchaguzi marekebisho kutoa nafasi ya uchaguzi wa mapema.

Waziri Mkuu anatarajiwa kuanza kunadi chama chake cha Conservatives. Aidha vyama vingine vimeanza kampeini kuhakikisha vinaongeza wingi wa wabunge.

Chama kitakachopata wabunge wengi kitaunda serikali na Waziri Mkuu atakua na wajibu kuamua mkondo ambao Uingereza itafuata katika kujiondoa Muungano wa Ulaya.

Bunge litavunjwa hapo mwezi Mei.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu