Mpango wa kudhibiti utoaji wa visa za kazi kwa wageni nchini Marekani kupitiwa upya.

In Kimataifa

Rais wa Marekani aliamua Jumanne hii usiku kutia saini amri ya kupitia upya mpango wa kudhibiti utoaji wa visa za kazi kwa wageni nchini Marekani maarufu kama H-1B. Lakini bunge la Congress litakabiliwa na kibarua kigumu kwa kupitisha sheria hiyo. Wabunge ndio wana uwez0 wa kuidhinisha au la sheria hiyo.

Rais Trump alichagua jimbo la Wisconsin, ambalo linakabiliwa na mdororo wa kiuchumi,akiomba kuwekeza katika jimbo hilo na kuajiri kwanza raia wa Marekani kabla ya mtu yeyote. Alitoa hotuba yake mbele ya bendera ya American katika jimbo la Wisconsin.

Sheria hii inayataka mashirika kufuata taratibu za Serikali katika kuondoa wafanyakazi wa kigeni kwenye mpango wa kuwania zabuni kwenye miradi ya serikali.

Sheria hii ina nia ya kutimiza ahadi yake aliyoitoa wakati wa Kampeni ya ”Marekani kwanza”.

Trump atatoa maelekezo kwa idara ya mambo ya ndani, sheria, usalama wa ndani na kazi na kupendekeza kufanyia mabadiliko mpango huo, ambao unawaruhusu waajiri nchini humo kuwapa wageni nafasi za kazi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu