Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika kozi waliyokuwa wanasoma chuoni hapo haitambuliki na Balaza la taifa la elimu ya ufundi NACTIVET.
Ombi hilo wamelitoa mbele ya Mkuu wa wilaya ya Mbeya Mh.Beno Malisa na Meneja wa kanda ya Nactivet Joha Fugutilo mara baada ya kuagiza chuo hicho kusimamisha mafunzo kutokana na kukiuka masharti ya uendeshaji huku Mh. Malisa akiagiza Nactivet kufanya uhakiki wa vyuo vilivyopo Wilayani Mbeya.
Katibu mtendaji wa Nactivet Tanzania kupitia kwa Meneja wa kanda ya nyanda za juu kusini Joha Fugutilo mbali na kuagiza chuo hicho kusimamisha utoaji wa mafunzo lakini pia amesema mmiliki asipotoa maelezo ndani ya siku saba chuo hilo kitafutiwa usajili wake
Kwa Upande wa wanafunzi wamedai wameiomba Serikali kusaidia kupata Suluhu ya jambo hilo kutokana na wengi wao kupoteza muda Wakiwa chuoni hapo na hasara Iliyojitokeza.
