Serikali kutengeneza ajira kwa Watanzania.

In Kitaifa

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amehudhuria kongamano la kitaifa la viwanda lililofanyika katika Ukumbi wa Kichangani mjini Iringa ambapo amesema nia ya serikali ya kuanzisha viwanda ni kutengeneza ajira kwa Watanzania.

Waziri Mwijage amesema hayo wakati wa maandalizi ya kuelekea kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Dunia, ambayo kitaifa yanatarajiwa kufanyika mkoani Iringa.

Mwijage amesema, Serikali imedhamiria kuongeza ajira kupitia sekta ya viwanda lakini pia uwepo wa viwanda umekuwa ukiongeza thamani ya mazao sehemu husika.

Amezitaka Serikali za mikoa na wilaya ziendelee kutenga maeneo kwa ajili ya viwanda.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana, Wazee na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama ameviasa viwanda nchini kufuata sheria za kazi kwa kuhakikisha usalama mahala pa kazi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu