Serikali yatangaza Ajira zaidi ya 21000

In Kitaifa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, ameridhia kibali cha kuajiri watumishi Elfu 21 na mia 2 wa Kada za Ualimu na Afya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Aprili 12, 2023 Waziri wa TAMISEMI Mhe Angellah Kairuki, amesema kuwa Idadi ya Watumishi watakaoajiriwa katika Kada za Ualimu ni Elfu 13 mia 1 na 30 ambao watafundisha katika shule za Msingi na Sekondari.

Aidha idadi ya watumishi watakaoajiriwa katika kada za Afya ni Elfu 8 na 70 ambao watafanya kazi katika Hospitali za Halmashauri, Vituo vya Afya na Zahanati.

Aidha Mhe Kairuki amesema waombaji wote wanatakiwa kuwa wahitimu wa mwaka 2015 mpaka 2022 kutoka katika vyuo vya elimu ya juu na vya kati kwenye fani ya Ualimu na Afya vinavyotambuliwa na Serikali.

Mhe Kairuki amesema waombaji wanatakiwa kuomba ajira kuanzia leo April 12 hadi 25 2023 saa 5:59 usiku.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu