“Vita itakoma Russia ikiondoa wanajeshi wake” – Zelensky

In Kimataifa

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenseky Jumanne amesema usitishwaji wa kweli na kamili wa uhasama utatokea ikiwa Russia itaondoa wanajeshi wake wote ndani ya Ukraine na kurejesha udhibiti wa eneo la Ukraine kwenye mpaka wake na Russia.

Akihutubia viongozi wa nchi za G20 kwa njia ya mtandao kwenye mkutano mjini Bali, Zelensky amesema kuchelewesha kumaliza mzozo inamaanisha vifo zaidi vya wanainchi wa Ukraine na vitisho zaidi kwa ulimwengu.

“Ninaamini sasa ni wakati ambapo vita haribifu vya Russia vinatakiwa kukomeshwa,” Zelensky amesema.

Matamshi ya kiongozi huyo wa Ukraine yanafuatia ziara yake jana Jumatatu katika mji uliokombolewa wa Kherson ambapo aliwaambia wanajeshi wa Ukraine kwamba nchi iko tayari kwa amani.

Rais wa Marekani Joe Biden, akizungumza Jumatatu kwenye mkutano na waandishi wa habari huko Indonesia, ameutaja ukombozi wa mji wa Kherson kuwa ushindi mkubwa kwa serikali ya Kyiv.

Lakini amesema washirika wa magharibi wanaoiunga mkono Ukraine hawatalazimisha suluhu kwa Ukraine kumaliza vita.

Alisema hakuna lolote litakalofanyika kuhusu Ukraine bila Ukraine kukubaliana nalo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu