“Vita itakoma Russia ikiondoa wanajeshi wake” – Zelensky

In Kimataifa

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenseky Jumanne amesema usitishwaji wa kweli na kamili wa uhasama utatokea ikiwa Russia itaondoa wanajeshi wake wote ndani ya Ukraine na kurejesha udhibiti wa eneo la Ukraine kwenye mpaka wake na Russia.

Akihutubia viongozi wa nchi za G20 kwa njia ya mtandao kwenye mkutano mjini Bali, Zelensky amesema kuchelewesha kumaliza mzozo inamaanisha vifo zaidi vya wanainchi wa Ukraine na vitisho zaidi kwa ulimwengu.

“Ninaamini sasa ni wakati ambapo vita haribifu vya Russia vinatakiwa kukomeshwa,” Zelensky amesema.

Matamshi ya kiongozi huyo wa Ukraine yanafuatia ziara yake jana Jumatatu katika mji uliokombolewa wa Kherson ambapo aliwaambia wanajeshi wa Ukraine kwamba nchi iko tayari kwa amani.

Rais wa Marekani Joe Biden, akizungumza Jumatatu kwenye mkutano na waandishi wa habari huko Indonesia, ameutaja ukombozi wa mji wa Kherson kuwa ushindi mkubwa kwa serikali ya Kyiv.

Lakini amesema washirika wa magharibi wanaoiunga mkono Ukraine hawatalazimisha suluhu kwa Ukraine kumaliza vita.

Alisema hakuna lolote litakalofanyika kuhusu Ukraine bila Ukraine kukubaliana nalo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu