Vitamin E inavyoweza kuboresha ngozi, kuondoa chunusi

In Afya

Kuna faida mbalimbali zitokanazo na matumizi ya vitamin kiafya hasa katika urembo
hususani katika vitamin C na Vitamin E ambazo huboresha muonekano wa ngozi yako.
Faida ya vitamin E katika ngozi hupunguza kasi ya ngozi kuzeeka, kupunguza madhara
ya mionzi ya jua kwenye ngozi lakini pia hupunguza muonekano mbaya wa makovu na
vipele.

Iwapo unataka kupunguza kupauka ngozi, madoa, makovu inashauriwa kuchanganya
mafuta ya Vitamin E na maji ya limao katika mafuta unayoyatumia pia unaweza
kuongeza rose water katika huo mchanganyiko.
Tumia pamba kupaka usoni na shingoni kaa na mchanganyiko huo kwa muda wa robo
saa kisha safisha uso tumia kwa siku 7 hadi 10 kuona mabadiliko pia itakusaidia kutibu
chunusi.
Unaweza kupaka usiku wakati wa kulala na asubuhi unasafisha uso wako kwa
kuchanganya kijiko kimoja cha ya mzaituni au mafuta ya nazi na mafuta kidonge kimoja
cha vitamini kisha unapaka kwa kuzunguka uso kwa kutumia vidole vyako.
Unashauriwa kutotumia mafuta ya Vitamin E bila ya kuchanganya na kitu chochote
kuyapunguza nguvu kunaweza kukuletea mchubuko wa ngozi laini kama ya kuzunguka
macho

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu