Waziri Nchemba atunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) UDSM.

In Kitaifa, Uchumi
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba jana Novemba 18, 2017 ameweka historia nyingine katika maisha yake baada ya kuhitimu masomo yake katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Waziri Nchemba amehitimu masomo yake ya Shahada ya Uzamivu (PhD) katika uchumi.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Nchemba ameweka picha zake na kuandika, anamshukuru Mungu kwamba amehitimu masomo yake ya PhD.
Katika kuandika tasnifu (thesis) yake, Waziri Nchemba aliandika kuhusu“Sterilization of Foreign Exchange Inflows in Tanzania: Extent and Effectiveness.
Katika kuandika tasnifu hiyo, Waziri Nchemba alisimamiwa na wakufunzi, Dr. Jehovaness Aikaeli na Dr. Eliab Luvanda.
Waziri Nchemba amehitimu masomo jana baada ya kutunikiwa shahada hiyo katika mahafali ya 47 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City ambapo leo ni kundi la kwanza.
Kundi la pili linatarajiwa kufanya mahafali yao katika ukumbi huo huo, Novemba 21 mwaka huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu