Wito watolewa kwa watendaji wa Mamlaka ya Maji safi jijini Dar es salaam(DAWASCO)

In Kitaifa

Wito umetolewa kwa watendaji wa Mamlaka ya Maji safi Jijini Dar es
Salaam (DAWASCO) kuongeza nguvu katika usambazaji wa huduma hiyo kwani
katika hatua ya uzalishaji imeonesha mafanikio.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa
Kitila Mkumbo wakati wa alipotembelea ofisi za Dawasco na kuzungumza
na watumishi wa Mamlaka hiyo, ambapo amewataka kuongeza kasi katika
usambazaji wa Maji na kuboresha miundombinu.

Aidha Profesa Mkumbo ametoa rai kwa Taasisi zisizolipia huduma hiyo
kusitishiwa mara moja kama ambavyo Agizo la Rais Magufuli kwa
wasiolipia huduma ya Umeme kusitishiwa.

Awali akiwasilisha ripoti ya hali ya utoaji huduma wa Mamlaka hiyo
Mkurugenzi Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema kuwa kwa sasa Mikoa ya
Dar es salaam na Pwani changamoto ya Huduma za maji safi zimepungua.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu